Kenna Wasike reviewed on 26 Apr 2026
Fumbo la Baba
Hii ni riwaya inayozungumzia mhusika anayegundua, kupitia kwa mazungumzo ya Sihaba na ndugu zake - Hidaya na Mashaka, kuwa Dkt Kirema, aliyedhani kuwa ni babake, kumbe si babake mzazi. Jaribio lake la kupata ukweli kutoka kwa mama, anapigwa. Hili linampa mawazo na mashaka mengi. Sasa anaingia katika safari ya kumsaka babake. Kusaka fasili yake. Anafunga safari kutoka Machewa kwenda Kemeloi kumsaka Bw. Katila ambaye ni babake mzazi.